KARIBU NG'S_CLINIC

JIFUNZE TOFAUTI YA UTE WA UZAZI NA UCHAFU UKENI


 *🌹Jifanyie Uchunguzi mwenyewe kujua tofauti ya  Ute wa uzazi na Uchafu.....*👇

*1. Ute wa Uzazi*
Huwa mweupe kama Yai 

Aina hii ya ute unakuwa unaashilia yafuatayo;
(I). Kwanza ni mweupe(Clear)
(II). Kuanguliwa kwa Yai kama ute huu unatoka siku za hatari za mzunguko wako. 
(III). Una mimba kama unatoka mda wote au mda mwingi.
(IV). Una afya nzuri ya uzazi kama unatoka katika kipindi maalumu.
(V). Hormone zako ziko vizuri

N.B
Ute huu uwe na sifa ya kuvutika na kuteleza na usiwe na harufu.



*2. Uchafu wa Rangi Ya Mawingu *

Huu ni uchafu na walio wengi huchanganya na ute wa uzazi.

Huu unaashilia una shambulio la bacteria. Mda mwingine unaweza kuwa mzito sana.

*3. Uchafu Mweupe sana*.

Mara nyingi uchafu huu unakuwa mweupe tofauti na ule wa wakati wa kuanguliwa kwa Yai unaovutika.

Unaashilia..
(I)Maambukizi ya fangus endapo unawasha  kutoa harufu.

*4. Uchafu ulio kama maziwa mgando, Kijani kuelekea  Njano*

Unaashilia.
(I). shida katika shingo ya kizazi ama PID sugu.
(II). ukuta wa uzazi umeshambuliwa na wadudu (PID)
(III).Ukiwa umeambatana na damu zaidi unakuwa unamaanisha kuna kitu kinajipachika kwenye ukuta wa uzazi hasa uvimbe kuota.
(IV). Magonjwa ya zinaa

*5. Uchafu wa kahawia/Nyekundu*

Unaashilia
(I).Upo period (hedhi)
(II).Kama nje ya tarehe zako za hedhi umaanisha  umeshambuliwa katika shingo ya kizazi na wadudu.
(III).Unapozidi kwa muda mrefu uashiria uwepo wa  uvimbe au Saratani n.k

Elimika kuhusu hili na endapo huwezi kutambua chochote wahi hospital kufanya uchunguzi zaidi.
Pia weka mazoea ya kutumia huduma zisizo na kemikali ili umalize shida kama hizi kwa usahihi zaidi Kuondoa chanzo husika cha Tatizo.

Kwa mawasiliano zaidi;
+255758077020
        Au
+255622198368

Post a Comment

0 Comments